NAFASI ZA KAZI WIZARA YA UCHUMI WA BULUU NA UVUVI

Posted: 2023-03-10 15:11:53
Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi kumi na nne (14) za kazi kwa ajili ya Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi - Zanzibar kama ifuatavyo:-

1.AFISA UVUVI MSAIDIZI DARAJA LA III (ZPSD-03) NAFASI (2) - UNGUJA
Sifa za Waombaji:
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu elimu ya Stashahada ya Kawaida (Ordinary Diploma) ya Uvuvi au fani inayolingana nayo kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2.AFISA SAYANSI YA MAZINGIRA DARAJA LA II (ZPSF – 02) NAFASI (1) – UNGUJA    
Sifa za Muombaji
Awe Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe na elimu ya Shahada ya Kwanza katika fani ya Sayansi ya Mazingira au fani inayolingana na hiyo kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3.AFISA MAABARA YA MIFUMO NA TABIA ZA BAHARI (OCEANOGRAPHY LABORATORY SCIENTISTS) DARAJA LA II (ZPSG-09) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Mifumo na Tabia za Bahari (Oceanography), Marine Science, Geography, Marine Geology au Fani inayolingana kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta kwa kufanya uchambuzi wa Mifumo na Tabia za Bahari
Awe na ujuzi wa kutumia taarifa za utambuzi wa mifumo ya Dunia (Earth observation systems) katika uchambuzi wa mifumo na tabia za bahari.
.
4.AFISA UTAFITI DARAJA LA I KATIKA FANI YA SAYANSI YA UVUVI (FISHERIES SCIENCES II) - NAFASI (1) UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46..
Awe amehitimu Shahada ya Pili katika fani za Fisheries Sciences, Marine Biology, Marine Science, Fisheries and Aquaculture kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 Awe na ujuzi wa kufanya Tafiti zinazohusiana na Uvuvi na Sayansi ya Uvuvi
Uzoefu wa kazi pamoja na machapisho za Tafiti katika Journal zinazotambulika (Peer Review Journals) ni sifa za ziada.
Ujuzi wa kuogelea na kuzamia (diving) ni sifa za ziada.

5.AFISA UTAFITI DARAJA LA II KATIKA FANI YA SAYANSI YA UVUVI (FISHERIES SCIENCES I) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani za Fisheries Sciences, Marine Biology, Marine Science, Fisheries and Aquaculture kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
 Awe na ujuzi wa kufanya Tafiti zinazohusiana na Uvuvi na Sayansi ya Uvuvi
Uzoefu wa kazi ni sifa za ziada.
Ujuzi wa kuogelea na kuzamia (diving) ni sifa za ziada.

6.AFISA UTAFITI DARAJA LA I KATIKA FANI YA UKUZAJI WA VIUMBE VYA BAHARINI (AQUACULTURE II) NAFASI (1)- UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Pili katika fani za Fisheries Sciences, Marine Biology, Marine Science, Fisheries and Aquaculture kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Awe na ujuzi wa kufanya Tafiti zinazohusiana na Ukuzaji wa Viumbe vya Baharini (Aquaculture)
Uzoefu wa kazi pamoja na machapisho katika Journal zinazotambulika (Peer Review Journals) ni sifa za ziada.

7.AFISA UTAFITI DARAJA LA II KATIKA FANI YA UKUZAJI WA VIUMBE VYA BAHARINI (AQUACULTURE I) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani za Fisheries Sciences, Marine Biology, Marine Science, Fisheries and Aquaculture kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Awe na ujuzi wa kufanya Tafiti zinazohusiana na Ukuzaji wa Viumbe vya Baharini (Aquaculture)
Uzoefu wa kazi pamoja na machapisho katika Journal zinazotambulika (Peer Review Journals) ni sifa za ziada.








8.AFISA UTAFITI DARAJA LA I KATIKA FANI YA MABADILIKO YA TABIANCHI (CLIMATE CHANGE II) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46..
Awe amehitimu Shahada ya Pili katika fani ya Mabadiliko ya Tabianchi (Climate Change) au Fani inayolingana kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Awe na ujuzi wa kufanya Tafiti zinazohusiana na Mabadiliko ya Tabianchi
Uzoefu wa kazi pamoja na machapisho katika Journal zinazotambulika (Peer Review Journals) ni sifa za ziada.

9.AFISA UTAFITI DARAJA LA II KATIKA FANI YA UHIFADHI WA BAHARI (MARINE CONSERVATION I) NAFASI (2) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Marine Conservation, Marine Ecology, Ecology, Forestry, Ecosystem Management, Coastal Management, Environment, Geography au fani inayolingana kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Awe na ujuzi wa kufanya kazi na jamii (community engagement skills)
Uzoefu wa kazi ni sifa za ziada.

10.AFISA UTAFITI DARAJA LA I KATIKA FANI YA IKOLOJIA YA BAHARI (MARINE ECOLOGY II) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Pili katika fani za Marine Ecology, Marine Biology, Marine Science, Ecology, Ecosystem Management au fani inayofanana nayo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Awe na ujuzi wa kufanya Tafiti zinazohusiana na Ikolojia ya Bahari
Uzoefu wa kazi pamoja na machapisho katika Journal zinazotambulika (Peer Review Journals) ni sifa za ziada.

11.AFISA UTAFITI DARAJA LA II KATIKA FANI YA IKOLOJIA YA BAHARI (MARINE ECOLOGY I) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani za Marine Ecology, Marine Biology, Marine Science, Ecology, Ecosystem Management au fani inyofanana nayo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Uzoefu wa kazi ni sifa za ziada.

12.AFISA UTAFITI DARAJA LA II KATIKA FANI YA MAIKROBAIOLOJIA (MICROBIOLOGY I) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46..
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Microbiology, Applied Microbiology au Biotechnology kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Uzoefu wa kazi ni sifa za ziada.

13.AFISA UTAFITI DARAJA LA II KATIKA FANI YA PARASITOLOJIA (PARASITOLOGY I) NAFASI (1) - UNGUJA
Sifa za Muombaji
Awe ni Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka 46.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Parasitology, Medical Parasitology, Applied Biology au fani inayofanana nayo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Uzoefu wa kazi ni sifa za ziada.

Jinsi ya Kuomba:

Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya Kielektronic kupitia Mfumo wa (Zan-Ajira) www.zanajira.go.tz kuanzia tarehe 09 Machi, 2023 hadi tarehe 24 Machi, 2023

Mfumo huo pia unapatikana katika tovuti ya Tume ya Utumishi Serikalini www.zanajira.go.tz
Muombaji anatakiwa kuainisha nafasi ya kazi anayoiomba.
Close
Close